Ni katika mchezo wa marudiano robo fainali ya mabingwa Ulaya
ambapo kwa hakika Man City wana kibarua kizito sana kwani wanatakiwa kuifunga
Liverpool bao 4-0 maana mechi iliyopita, Man City walibamizwa 3-0 pale Anfield
mjini Liverpool.
Wachezaji wa Timu ya Man City wakishangilia goli lililofungwa na Mchezaji Sergio Kun Aguero hivi karibuni. |
Kiungo wa City, Fernandinho mwenye umri wa miaka 32 anasema lile
juma gumu lililowakabili la kuchapwa kila walikoenda sasa limeisha na ni wakati
sasa wa wachezaji wazoefu kuchukua nafasi yao na kuliongoza Jahazi.
Tangu Man City walipopoteza pale Anfield jumatano, pia katika ligi
walichapwa 3-2 na Manchester United.
Liverpool ilifunga mara tatu ndani ya dakika 19 za kipindi cha
kwanza katika mzunguko wa kwanza.
Ikiwa upande wa Jurgen Klopp utaweza kushinda katika Uwanja wa
Etihad, City watalazimika kushinda angalau mara tano ili kuendelea kufikia
nafasi ya nne.
Ni Timu mbili pekee katika historia ya Champions League ambazo
zimewahi kujikwamua kutoka katika deni la magoli matatu au Zaidi katika kipindi
cha mtoano. Sawa na deni analokabiliana nalo Man City.
Wachezaji wa Liverpool wakishangilia mojawapo ya magoli waliyoyafunga msimu huu, 2018 |
Deportivo La Coruna ikiwa nyuma ya AC Milan 4-1 mwaka 2004
walifanikiwa kupindua matokeo kwa 4-0 in katika mechi ya marudiano.
Katika siku za hivi karibuni, ni Barcelona iliyobadilisha
matokeo ya 4-0 dhidi ya Paris St-Germain kwa kushinda 6-1 katika mechi ya
marudio uwanja wa Noe Camp msimu uliopita.
Katika mchezo mwingine wa marudiano robo fainali ya mabingwa
Ulaya, Roma itashuhudiwa wakikwaana na Barcelona katika uwanja wa Stadio
Olimpico.
Nyota wa klabu ya soka ya Barcelona Luis Suarez, Lionel Messi na Moussa Dembele wakishangilia goli waliloifungia klabu hiyo hivi karibuni. |
Meneja wa Roma Eusebio di Francesco amekiri kwamba kwa hakika
kukutana na Barcelona anakutana na alichokiita Mashine lakini anabaki na
matumaini makubwa.
Waitaliano hao wanakutana na Wahispania huku waitaliano wakiwa
na hasira za kuchapwa bao 4-1 katika mzunguko wa kwanza.
Pia Roma walichapwa 2-0 na Fiorentina aliyeko nafasi ya saba na
sasa wana point 21 nyuma ya viongozi wa Seria A Juventus
Wachezaji wa AS Roma kwenye moja ya michezo yao ya hivi karibuni kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa ya Ulaya, 2018 |
Katika hali ya tofauti, Barcelona wakiwa na Lionell Messi wako
pointi 11 juu na bado Meneja wao Ernesto Valverde pamoja na kuwa watakuja na
faida ya magoli matatu kibindoni bado amesema mechi hii dhidi ya Roma hawataichukulia
kawaida na kwa hakika wataingia Uwanjani kama vile matokeo ni 0-0.
Katika upande wa Championship Cardiff City wataondoka katika
nafasi ya pili kama watashindwa kuwapiga Aston Villa na iwapo pia Fulham
itawachapa Reading wanaopambana kujiokoa kushuka daraja.
Source: BBC