UMUHIMU WA MAZOEZI - MALIKITA SAFARI FITNESS

Recent Posts

test

Wednesday 7 February 2018

UMUHIMU WA MAZOEZI

                                      UMUHIMU WA MAZOEZI KWA VIUMBE HAI WOTE

Mazoezi ni  muhimu  saana kwa viumbe hai wote. na wote hua tunafanya mazoezi kulingana na hali na mazingira.wanyama kwa kua hawajapewa akili hua wanafanya mazoezi pasipo kujua kama wanafanya mazoezi au la . vivyo hivyo hata sisi wanadamu kuna kipindi tunafanya mazoezi pasipo kujua kama tuna fanafanya mazoezi 







.na hicho kipindi ni pale tunapokua watoto kwani mungu ametutengenezea mazingira ambayo kipindi hicho kila mmoja lazima apitie kwenye michezo mingi na kukimbia bila sababu. tunapokua na akili yaani umri wa kujitambua ndio tunaamrishwa na kuambiwa umuhimu wa mazoezi. Kwani jambo hili japo somo lake  linafundishwa kuanzia shule za awali yaani chekechea kuhusu umuhimu wa mazoezi lakini jamii bado ni wagumu kukubaliana na elimu hiyo au kutekeleza .lakini kutokukubali kwao haimaanishi kua hayatokei madhara yatokanayo na kukataa kwao.la hasha madhara yake ni makubwa na yanatia simanzi kwa kiwango kikubwa sana. kwani wataalam wa afya wanasema 27% ya vifo vinavyotokea  hasa nchini kwetu ni vifo vinavyoweza kuepukika endapo tu watu watabadili tabia ya kupenda kufanya mazoezi .wewe mwananchi serikali yetu  kupitia kwa mama yetu mpendwa makamu wa raisi mama samia suluh imegundua kua watu wake wanaelekea kwenye  shimo. ikapelekea kuzindua siku maaalumu kwa ajili ya watu wote wafanye mazoezi .serikali ilizindua siku hiyo ili kukumbusha uwe na utamaduni wa kufanya mazoezi kwa faida ya kwako na jamii iliokuzunguka lakini cha ajabu watu wengi uzinduzi huu wanafananisha na uzinduzi wa barabara au uzinduzi mwingine kwani kiukweli bado watu hawajazinduka kabisa .unapomuambia mtu kuhusu mazoezi analeta visingizio vingi lakini sababu zote hizo hazina mashiko .kumbuka uzinduzi huu ni kuzindua akili yako ushike njia sahihi ya afya mwenye jukumu la kutunza afya ni jukumu la kila mtu mwenyewe binafsi wala sio jukumu la mama samia suluh wala sio la rais wetu magufuli.hakika kuumbwa kwetu hapa duniani ni kwa ajili ya kumtumikia mwenyezi mungu maana ya kumtumikia ni kufuata maagizo yake kwa hiyo mazoezi pia ni sehemu ya maagizo kwetu kutoka kwake kwani .mwili usipofanya mazoezi ni sawa na chuma kukaa bila kutumika lazime kishike kutu na kupelekea kuzeeka .hivyo ukishiriki mazoezi unategemea kupata faida mbili kwa wakati mmoja kwanza utapata Baraka  kwa sababu umetekeleza kanuni alizotuwekea .na faida ya pili utaboresha afya yako.pia usipofanya mazoezi unapata hasara mbili kwa wakati mmoja kwanza utapata dhambi kwa kua umekataa maamrisho ya mwenyezi mungu pia utapata afya mbovu na ukipoteza maisha chanzo chake kikibainika kwa sababu ya kutofanya mazoezi bila shaka hautakua tofauti na mtu aliepoteza maisha kwa kujinyonga kwani Yule aliejinyonga kwa kamba katumia maamuzi ya ghafla lakini mtu aliekufa kwa maradhi nyemelezi amejinyonga taratibu kwa muda mrefu.kwa hiyo acha kufuata kamba utakayotumia kujinyonga kwa kufuata njia sahihi ya afya NAMALIZIA KUSEMA ZINDUKA……ZINDUKA……ZINDUKA…….MAMA SAMIA  SULUH  AMEKUZINDUA