April 2018 - MALIKITA SAFARI FITNESS

Recent Posts

test

Monday 16 April 2018

TETESI ZA SOKA ULAYA WIKI HII

April 16, 2018
TETESI ZA SOKA ULAYA WIKI HII



Thomas Lemar
Thomas Lema

Image
caponaco yaangalia kumchukua kiungo kutoka Ufaransa Thomas Lemar msimu wa majira ya joto. Timu za Arsenal na Liverpool pia zimeonekana kumtupia jicho Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 22.(Telefoot)
Mshambuliaji wa LA Galaxy Zlatan Ibrahimovic anasema ananafasi kubwa ya kuchezea timu ya Sweden katika michezo ya kombe la dunia nchini Urusi,licha ya kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 36 amestaafu kucheza soka ya kimataifa tangu 2016 (Sun)


Aberdeen manager Derek McInnes
Derek McInnes
Image caption
Aliyekuwa mchezaji wa West Brom,Derek McInnes na mkuu wake wa Baggies Tony Mowbray ni miongoni mwa waliopendelewa kupata kazi ya kuwa meneja wa West Brom (Mirror)
Rais wa Roma James Pallotta anasema klabu hio 'haina nia ya kumuuza' mlinda mlango kutoka Brazil Alisson(25), ambaye ana aminiwa kuhamia Liverpool.
Mlinzi wa Chelsea Antonia Rudiger,25, anasema hajajua sababu ya yeye kutocheza dhidi ya Southampton, akiongezea kuwa alikuwa 'tayari kabisa' kwa ajili ya mechi ya Jumamosi


Newcastle goalkeeper Martin Dubravka catches the ball
Dubravka
Haki miliki ya picha
Image caption

Newcastle wanajipanga kumsajili mlinda mlango Martin Dubravka kwa mkataba endelevu. Mslovak huyo,29, aliungana na Magpies kwa kukopeshwa na timu ya Sparta Prague mwezi Januari. (Express)
Mkuu wa Newcastle Rafael Benitez anatarajia kufanya mazungumzo na mmiliki wa timu, Mike Ashley kabla ya kusaini mkataba mpya . Benitez anataka kuhakikisha kuwa kuna fedha za kutosha za kufanyia usajili wa wachezaji katika msimu wa majira ya joto kabla ya kuingia katika klabu hio.(Telegraph)


Wilfried Zaha
WILFRED ZAHA
Meneja wa Crystal Palace Roy Hodgson anasema anajutia kwamba hakuweza kumshawishi winga wa Eagles Wilfried Zaha (25) kuchezea timu ya England dhidi ya Ivory Coast. (Mail)
Arsenal, Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Tottenham wanampango wa kurejea juhudi za kupata fedha zaidi kutoka kwa marupurupu wanaolipia nchi za nje kutangaza mechi za Premier League. (Mail)
Mshambuliaji wa Liverpool kutoka Misri Mohamed Salah, 25, anasema kushinda Champions League ni muhimu zaidi kuliko yeye kuwa mfunga goli bora zaidi wa Premier League na kupata tuzo ya Golden Boot. (Guardian)
Credit: BBC

Tuesday 10 April 2018

Manchester City wataweza kulipa kisasi kwa Liverpool UEFA leo?

April 10, 2018
Manchester City wataweza kulipa kisasi kwa Liverpool UEFA leo?

Ni katika mchezo wa marudiano robo fainali ya mabingwa Ulaya ambapo kwa hakika Man City wana kibarua kizito sana kwani wanatakiwa kuifunga Liverpool bao 4-0 maana mechi iliyopita, Man City walibamizwa 3-0 pale Anfield mjini Liverpool.
Wachezaji wa Timu ya Man City wakishangilia goli lililofungwa na Mchezaji Sergio Kun Aguero hivi karibuni.
Kiungo wa City, Fernandinho mwenye umri wa miaka 32 anasema lile juma gumu lililowakabili la kuchapwa kila walikoenda sasa limeisha na ni wakati sasa wa wachezaji wazoefu kuchukua nafasi yao na kuliongoza Jahazi.
Tangu Man City walipopoteza pale Anfield jumatano, pia katika ligi walichapwa 3-2 na Manchester United.
Liverpool ilifunga mara tatu ndani ya dakika 19 za kipindi cha kwanza katika mzunguko wa kwanza.
Ikiwa upande wa Jurgen Klopp utaweza kushinda katika Uwanja wa Etihad, City watalazimika kushinda angalau mara tano ili kuendelea kufikia nafasi ya nne.
Ni Timu mbili pekee katika historia ya Champions League ambazo zimewahi kujikwamua kutoka katika deni la magoli matatu au Zaidi katika kipindi cha mtoano. Sawa na deni analokabiliana nalo Man City.
Wachezaji wa Liverpool wakishangilia mojawapo ya magoli waliyoyafunga msimu huu, 2018
Deportivo La Coruna ikiwa nyuma ya AC Milan 4-1 mwaka 2004 walifanikiwa kupindua matokeo kwa 4-0 in katika mechi ya marudiano.
Katika siku za hivi karibuni, ni Barcelona iliyobadilisha matokeo ya 4-0 dhidi ya Paris St-Germain kwa kushinda 6-1 katika mechi ya marudio uwanja wa Noe Camp msimu uliopita.
Katika mchezo mwingine wa marudiano robo fainali ya mabingwa Ulaya, Roma itashuhudiwa wakikwaana na Barcelona katika uwanja wa Stadio Olimpico.
Nyota wa klabu ya soka ya Barcelona Luis Suarez, Lionel Messi na Moussa Dembele wakishangilia goli waliloifungia klabu hiyo hivi karibuni.
Meneja wa Roma Eusebio di Francesco amekiri kwamba kwa hakika kukutana na Barcelona anakutana na alichokiita Mashine lakini anabaki na matumaini makubwa.
Waitaliano hao wanakutana na Wahispania huku waitaliano wakiwa na hasira za kuchapwa bao 4-1 katika mzunguko wa kwanza.
Pia Roma walichapwa 2-0 na Fiorentina aliyeko nafasi ya saba na sasa wana point 21 nyuma ya viongozi wa Seria A Juventus
Wachezaji wa AS Roma kwenye moja ya michezo yao ya hivi karibuni kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa ya Ulaya, 2018
Katika hali ya tofauti, Barcelona wakiwa na Lionell Messi wako pointi 11 juu na bado Meneja wao Ernesto Valverde pamoja na kuwa watakuja na faida ya magoli matatu kibindoni bado amesema mechi hii dhidi ya Roma hawataichukulia kawaida na kwa hakika wataingia Uwanjani kama vile matokeo ni 0-0.
Katika upande wa Championship Cardiff City wataondoka katika nafasi ya pili kama watashindwa kuwapiga Aston Villa na iwapo pia Fulham itawachapa Reading wanaopambana kujiokoa kushuka daraja.
Source: BBC